Mshambuliaji wa Chelsea Fernando Torres akishangilia goli alilofunga dhidi ya Rubin Kazan |
Kocha wa Chelsea amesema ameridhishwa sana na kiwango
kinachooneshwa na Torres katika michezo ya hivi karibu na ana uhakika
ataendelea kusalia kwenye kiwango chake na kufunga magoli zaidi.
Benitez ambaye anapigana ili kuhakikisha Chelsea inatwaa taji la kombe la FA na Kombe la Europa amesema Torres amerea kwenye kiwango wakati muafaka ambapo mchango wake unahitajika zaidi.
Licha ya Torres kutofunga goli katika michezo ya Ligi Kuu nchini Uingereza tangu tarehe 23 ya mwezi Desemba lakini Benitez haoneshi kukerwa na hilo na badala yake kufunga kwake kwenye Europe kunampa faraja.
Benitez amepongeza hatua ya Torres kupigana kufa na kupona kutaka kuwa kwenye kikosi cha kwanza na matunda yake yameanza kuonekana baada ya kufunga katika mchezo huo wa Robo Fainali tena magoli mawili.
Kocha huyo wa muda amesema wataendelea kumtumia Torres pamoja na Demba Ba katika safu ya ushambuliaji kuhakikisha wanashinda mataji mawili wanayoyawania msimu huu kwa udi na uvumba.
Benitez ambaye anapigana ili kuhakikisha Chelsea inatwaa taji la kombe la FA na Kombe la Europa amesema Torres amerea kwenye kiwango wakati muafaka ambapo mchango wake unahitajika zaidi.
Licha ya Torres kutofunga goli katika michezo ya Ligi Kuu nchini Uingereza tangu tarehe 23 ya mwezi Desemba lakini Benitez haoneshi kukerwa na hilo na badala yake kufunga kwake kwenye Europe kunampa faraja.
Benitez amepongeza hatua ya Torres kupigana kufa na kupona kutaka kuwa kwenye kikosi cha kwanza na matunda yake yameanza kuonekana baada ya kufunga katika mchezo huo wa Robo Fainali tena magoli mawili.
Kocha huyo wa muda amesema wataendelea kumtumia Torres pamoja na Demba Ba katika safu ya ushambuliaji kuhakikisha wanashinda mataji mawili wanayoyawania msimu huu kwa udi na uvumba.
Post a Comment