Home » , » MWANADADA SHILOLE AJITOA FAHAMU SERENGETI FIESTA 2013 TABORA

MWANADADA SHILOLE AJITOA FAHAMU SERENGETI FIESTA 2013 TABORA

Written By shebby on Tuesday, August 27, 2013 | 4:55 AM


Msanii  wa muziki wa Bongo fleva na filamu Shilole akiimba huku akiwa amelala chini ndani ya Viwanja vya Al-Hassani Mwinyi mjini Tabora.
Baadhi ya mashabiki waliojitokeza kucheza jukwaani,wakionesha umahiri wao wa kukata nyonga mbele ya umati wa wakazi wa mji wa Tabora na vitongoji vyake,waliojitokeza kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013 ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi.
  Raisi wa Manzese,kutoka kundi la Tip Top Connections,Madee akifanya yake jukwaani.
Mashabiki wakiitikia kwa pamoja huku mikono yao wakipunga hewani.
Mdogo wa Ali Kiba, Abdul Kiba, akiimba mbele ya umati mkubwa wa wakazi wa mji wa Tabora waliojitokeza kwa wingi katika Tamasha la Serengeti Fiesta 2013 ndani ya Viwanja vya Al- Hassani Mwinyi.
Msanii wa Bongo Fleva Amini Minyimkuu, akionyesha uwezo wake katika kulitawala jukwaa katika tamasha la Serengeti Fiesta 2013
Baba Levo akipagawisha
Shangwe zilitawala namna hii
Msanii wa muziki wa Dansi Bongo,Christian Bella akiwaimbisha mashabiki wake wa muziki wa dansi  kwenye tamasha la Serengeti Fiesta, ndani ya  uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora.
Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa Tabora waliojitokeza kwenye Serengeti Fiesta 2013
Msanii wa muziki wa bongofleva,Rachael akicheza jukwaani na mmoja wa madensa wake
Share this article :

Post a Comment

 
thanx to : my family | bongoclan | shebby.c
Copyright © 2011. BONGODASH - All Rights Reserved
imetengenezwa na blogdesinerimepigwa chapa na mchakato
Proudly powered by Blogger