umati wa watu wafurika kusikiliza rufaa ya lema
![]() |
WAFUASI WA CHADEMA |
Kesi ya aliyekuwa mbunge wa jimbo la Arusha mjini Ndugu 'Godbless Lema'
imesikilizwa mapema leo Septemba 20 kwenye mahakama ya rufani jijini
Arusha na jaji mkuu 'Othman Chande'. Kesi hiyo iliyofunguliwa na Mbunge
huyo kupinga kutenguliwa kwake ubunge na mahakama kuu ilisikilizwa kwa
takribani saa 2 kabla ya kuahirishwa ambapo 'Lema' aliwasilisha
mahakamani hapo hoja 18 za kupinga hukumu ya awali ya kesi yake.
Ilifahamika hata kabla ya kesi
hiyo kusikilizwa mawakili wa pande zote mbili (Chadema na Ccm) waliandika barua zilizofika mahakamni hapo kuomba kuahirishwa kwa kesi hiyo kutokana na mawakili 'Tundu Lissu' anayemtetea Lema na kaka yake 'Alute Mughwai' anayewatetea walalamikaji kufiwa na baba yao mzazi. Kesi hiyo ambayo ilihudhuriwa na wafuasi wengi wa chama cha Chadema waliomsindikiza 'Lema' imeahirishwa hadi tarehe 2 Oktoba mwaka huu itakaposikilizwa tena.
hiyo kusikilizwa mawakili wa pande zote mbili (Chadema na Ccm) waliandika barua zilizofika mahakamni hapo kuomba kuahirishwa kwa kesi hiyo kutokana na mawakili 'Tundu Lissu' anayemtetea Lema na kaka yake 'Alute Mughwai' anayewatetea walalamikaji kufiwa na baba yao mzazi. Kesi hiyo ambayo ilihudhuriwa na wafuasi wengi wa chama cha Chadema waliomsindikiza 'Lema' imeahirishwa hadi tarehe 2 Oktoba mwaka huu itakaposikilizwa tena.

'Lema' akiwasili mahakamani,

Askari polisi wakidumisha usalama maeneo ya Arusha wakati wafuasi
wakimsindikiza Lema,

Umati wa wakazi wa Arusha waliofika eneo la Mahakama Kuu kusikiliza
rufaa hiyo.

Wananchi wakiwa nje ya ofisi ya chama wanamsikiliza lema.
Post a Comment