Siku moja baada ya Klabu ya Arsenal ya nchini Uingereza kupata kipigo
cha magoli 3-1 kwenye Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya kutoka kwa Bayern
Munich kiungo wake Jack Wilshere amekataa kuelekeza lawama kwa Kocha wao
Arsene Wenger. Kiungo huyo Kinda Mahiri wa
Arsenal Wilshere amesema Kocha Wenger hapaswi kunyooshewa kidole cha
lawama kwa matokeo hayo na badala yake wachezaji wenyewe inabidi
wawajibike kwa hilo.
Wilshere amesema kwa kipindi cha miaka 16 Wenger amefanyakazi yake
ipasavyo hivyo hakuna sababu ya aina yoyote ya kuhoji kile ambacho
anakifanya na huu ni wakati wa wachezaji kuonesha uwajibikaji wao.
Kiungo huyo amesema Kocha Wenger alifanya kazi yake vizuri nje ya
uwanja na sehemu ambayo ilisalia ilikuwa ni kwa wachezaji wenyewe
kuwajibika na kupata matokeo mazuri lakini haikuwa hivyo.
Wilshere amesema walianza mchezo huo vibaya na ndiyo maana wakajikuta
wakiruhusu magoli mawili kwenye kipindi cha kwanza na walipoarekebisha
makosa wakacheza vizuri na hata kupata goli moja.
Kinda huyo wa Kiingereza amesema lazima waweka wazi ukweli ambao kwa
Klabu kama Arsenal haiwezi kupata matokeo mazuri kwa Timu bora kama
Bayern Munich ambayo imesheheni wachezaji mahiri.
Kwa upande wake Wenger amesema wanakazi ngumu mbele yao ili waweze
kufuzu katika hatua ya Robo Fainali kutokana na kuruhusu magoli kwenye
mchezo huo wa kwanza waliocheza nyumbani.
Wenger hakusita kusema chochote kinaweza kikatokea kwa kipindi cha
majuma mawili hayajayo na huenda wakapata nafasi ya kutinga Robo Fainali
japokuwa ukweli ni vigumu sana kwao.
Arsenal imejiweka kwenye mazingira magumu ya kufuzu katika hatua ya
Robo Fainali huku ikiwa na kumbukumbu ya kuondolewa kwenye Kombe la
Chama Soka nchini Uingereza FA baada ya kupokea kipigo kutoka kwa
Blackburn Rovers.
Post a Comment