Dudubaya alisema kuwa mbali na muziki kuna vitu alikuwa akifanya ambavyo aliona kuwa hawezi kuvifanya huku anafanya muziki.
Akiongea kwa njia ya simu kutoka Mwanza, Dudubaya
aliyewahi kutamba na nyimbo kama 'Nakupenda', 'Ruka Ruka', 'Mwanangu
huna Nidhamu' alisema biashara anazofanya ambazo hakuwa tayari

kuzitaja, zinamfanya asafiri sana mikoani na muda mwingi anakuwa Mwanza kwa sababu ndo kituo kikubwa cha biashara hizo.

kuzitaja, zinamfanya asafiri sana mikoani na muda mwingi anakuwa Mwanza kwa sababu ndo kituo kikubwa cha biashara hizo.
Dudubaya alikanusha taarifa ambazo ziliwahi
kusambaa kwenye mitandao ya jamii kuwa bado anaendelea na tabia yake ya
ugomvi na akiwa Mwanza aliwahi kumpiga mtangazaji wa kituo kimoja mkoani
humo.
"Niko kwenye muziki toka mwaka 1997, sijawahi
kumpiga mtangazaji yeyote.Kuna hata baadhi ya waandishi wa habari
walikuwa wanaandika skendo ambazo hazikuwa za kweli lakini sikuwahi
mpiga yeyote wakati wengine nawajua.Nawaheshimu sana watangazaji, MaDj
na waandishi wa habari, mimi siku hizi sio mgomvi tena kama zamani",
alieleza Dudubaya.
Aliendelea kueleza kuwa kilichopelekea habari
kusambaa kuwa kapiga mtangazaji ni mambo ya tofauti binafsi huko Mwanza
na wala si ya kimuziki kama ambavyo habari zilisambaa.
Dudubaya anasema kwa muda ambao alikuwa kimya
alikuwa akifikiria afanye muziki wa aina gani ili aweze kuwateka
mashabiki wake kama ilivyokuwa awali.
Wimbo wa mwisho Dudubaya kutoa ilikuwa ni Mwaka
2011 ulikuwa unaitwa 'Mdundo'. Alisema mwaka 2013 amerudi rasmi kwenye
na wimbo wake mpya utatoka mwishoni mwa wiki hii. Wimbo huo umerekodiwa
hukohuko Mwanza katika studio inayoitwa One Love FX chini ya produza
Tiddy Hotter.
Post a Comment